Monday, December 08, 2008

Software Platform

I have been following new softwares as they were updated from Filehippo and come to love it, sometimes back I came accross free and open source applications website softpedia.com.

It was recently that I learn on OpenDesktop and freshmeat and GnomeFiles. I haven't spent enough time in these sites but they look promising and need recommending.

After looking at some of of these you may drop your comments on which you think is the best.

Saturday, September 13, 2008

Hapa ndipo mahala pa kujisetiri mpaka jua lionekane tena. Kitanda cha kuning'inia wataka nini tena?

Nani kasema majani ya shida huku? Eneo lote limezungukwa na nyasi ndefu mno, hivyo hakuna haja ya kuzileta nyumbani tena. Mara nyingi wadudu wanazifuata, nani ataka karaha ya kufukuza siafu kila siku?

Karibuni kwesui katika wilaya ya Kilindi, Tanga.
Sehemu ya kujisetiri kwa wanafamilia wa Kwesui na wageni wao. Inadhaniwa kuwa mtu akiwajisetiri hapo muda wa mchana huwa haonekani ndio maana wenyeji wameona uvivu kufunika kwa nyasi.

Nyasi za nini wakati sayansi ishamaliza yote? Harufu na watoto kucheza karibu ndio tatizo tu. Kwani wahenga walisema usichezee shilingi ....
Nyumba ya mkazi mmoja wa Kwesui, Kilindi tulipomtembelea hivi karibuni
Si Kaburi la mfalme hilo ila ni alama ionyeshayo kanisa tu

Alama ya kanisa pale Tunduru, wilaya maarufu kwa kuwa na Simba wa mjini. Wadau nisaidieni nini maana ya kuweka alama hii sehemu kama hii.
Posted by Picasa
Nikiwa mbele ya Kanisa Katoliki la Kambi ya Tisa kijijini Kwaluguru katika wilaya ya Kilindi, Tanga.

Kinachovutia kwenye kanisa hili lililo porini ni kukosa altare na si rahisi kujua mbele ni wapi. Ni ama kwenye msalaba au njia ya kufika kanisa ilipo ndio huwa mbele ili wachelewaji waonekane.

Maandhari yake ni safi kabisa, yanafagiliwa na kufanyiwa usafi. Ila hali ya umasikini uliopo kitongojini hapa ni vigumu kabisa kuamini kama kuna mahekalu katika nchi hii.
Posted by Picasa

Friday, February 01, 2008

Mauaji ya Kenya

Leo nimeona ni bora nikatoka kidogo na kueleleza maoni na masikitiko yangu kuhusu mauaji yanayoendelea kule Kenya.

Mwaka 1994 tulishuhudia mauaji makubwa katika karne iliyopita yaliyohusisha chuki za kikabila kule Rwanda. Nchi nyingi duniani ama zilikaa kimya au kuunga mkono kwa njia moja ama nyingine.

Ni jambo la kushangaza sana kuona nchi zikikaa kimya hali zikijua kabisa yanayoendelea. Labda serikali ikihusika kwenye uuaji wa raia wake wenyewe, sote twaona aibu kuikosoa. Tutakaa kimya kama vile hatusikii.

Mara kwa mara nimeona Marekeni ikijaribu kuingilia baadhi ya migogoro hapa duniani. Kile nilichosikia ni kulinda maslahi yake katika nchi hizo. Hili laweza kuwa kweli, ila maisha ya watu ni maslahi ya nani? Nani haswa atakiwaye kuingilia kati pale mmoja mwenye nguvu zaidi akim'ua mnyonge?

Laiti kama wote wangekuwa wananguvu za kijeshi walao za kushindana, sidhani kama kungekuwa na shida. Lol, hapana … nimekosea. Nishuhudiavyo mara kulipotokea hali ya aina hiyo, na kama serikali iliyo madarakani inaonekana kuelemewa. Mara moja majirani na marafiki watapeleka majeshi yao kuokoa serikali. Wale wenye silaha wataitwa waasi na watu wasiostahili kabisa.

Sasa maslahi ni Serikali zilizo madarakani ama nini? Lazima kuna jambo wafanyalo sirini. Mie sijui, weye ujuaye naomba unihabarishe.

Wednesday, January 30, 2008

 
 
 
 

Nimefurahishwa sana na matumizi makubwa ya pikipiki katika mji huu. Hata kama una gari utajitahidi tu kusafirisha mizigo kwa kutumia tuk-tuk.

Kule Songea naona walikuwa wanaelekea kuwa kama hawa kwani yeboyebo zao zilivoma sana.

Pengine ni umasikini unaosababisha haya yote, ila ni bora zaidi kama usafiri huu utakuwa salama, sheria za barabarani zikaheshimiwa na wao wakalindwa.
Posted by Picasa
 

Kitimoto nao wanasafirishwa kama kuku.
Posted by Picasa
 


Usafifi si mpaka uwe na pick-up, laiti guta lingekuwepo ni biashara tu.
Posted by Picasa





Nilipo kuwa Namtumbo na Tunduru katikati ya mwaka 2007.

Katika Ushoroba wa Selous - Niassa, kama waitavyo uchochoro (corridor) wa wanyama pori kati ya Mbuga za Selous ya Tanzania na Niassa ya Msumbiji.
Helo waungwana, nimerudi tena kwenye Blogu baada ya kitambo kirefu.

Maoni, mawazo, ushauri na maswali yanakaribishwa sana.