Tuesday, April 21, 2009

Nipo kwenye daraja la Kilyamatundu-Kamsamba (huko kwenye bonde la ufa)
Posted by Picasa
Hello waungwana.
Hivi karibuni nilikuwa kule Bondeni kwenye bonde la ufa Rukwa nikiangaza sehemu za kupitisha daraja juu ya mto mkubwa wa Momba. Nimeishi kwenye kijiji cha Tululu.

Nilifanikiwa kupitia vijiji vya Chombe, Tululu, Kipeta na Kilyamatundu vya wilaya ya Sumbawanga. Hata hivyo nilifanikiwa kuvuka mto sehemu mbili za Tululu na Kilyamatundu na kwenda wilaya ya Mbozi kwenye vijiji vya Mkulwe na Kamsamba (walivuma kwa kuchuna ngozi za watu).

Vijiji vya Kilyamatundu na Kamsamba vinaunganishwa na daraja la waya (liite hivyo) japo vikajagio ni vya mbao. Daraja hili lilinishangaza sana kwa jinsi lilivyo refu na uundaji wake ulivyokuwa wa kitaalam. Heko kwa wabunifu wa daraja hili.

Zifuatazo ni baadhi ya picha za daraja hili. Toa maoni.